Mpira wa kengele au ‘Goal ball’ ni mchezo
HISTORIA
ulioanzishwa na raia wa Australia, Hanzi Lorenzen na raia wa Ujerumani, Sepp Reindle mwaka 1946 kwa ajili ya kuwasaidia askari waliopigana vita ya pili ya dunia na kupata matatizo ya macho.Na kuwa mchezo maarufu unao chezwa na watu wenye ulemavu wa uoni Mfano katika mashindano makubwa ya Par Olympic
MCHEZO
Washiliki
huchezwa na washiriki watatu wasioona, au wenye uono hafifu ambao hufungwa vitambaa usoni, ambapo mchezaji atalazimika kuucheza kwa kutumia hisia za kengele kwani mpira wenyewe unapoburuzika ni rahisi kuusikia mlio wa kengele hivyo na utazuiwa kwa kuudaka.
MUDA.
unaochezwa kwa dakika 24, dakika 12 kila upande na dakika 5 za mapumziko
UWANJA.
goli linalotumika kwa kila upande lina upana wa mita 9 wakati uwanja mzima una ukubwa wa mita 18 sawa na uwanja unaotumika kwa ajili ya mpira wa wavu (volleyball).
VIFAA.
Vipo vifaa mbalimbali kwa ajili ya mchezo huu miongoni ni
- Mpira wa kengele
- Firimbi
- Kitambaa/viraka vya jicho/Miwani
- Sale
- Zuria
- Koni
%20(21).jpeg)
%20(22).jpeg)