Bwana Twiga
Bwana Twiga, Bwana Twiga,
Kwa nini shingo yako ni ndefu sana?
Ulipoumbwa ilikuwa ni utani,
Au shingo yako ni kosa kweli?
Au unahitaji kuifikia
Mijani ya miti mirefu, mirefu sana?
Haiingii akilini, maana unapokunywa
Lazima upige magoti chini kabisa!
Mbuzi Mkongwe
Rose ana mbuzi.
Ni mbuzi mkongwe.
Ana mbuzi watoto.
Rose aliwauza mbuzi watoto.
Nina Chura Mdogo
Nina chura mdogo,
Jina lake ni Tiny Tim.
Nilimweka kwenye bafu,
Kuona kama anaweza kuogelea.
Alikunywa maji yote.
Alikula sabuni yote.
Na alipojaribu kuzungumza,
Alikuw
a na kiputo kooni.
YALIYOMO
HADITHI ZA WATOTO

.jpeg)
.jpeg)