Magonjwa ya Akili ni Nini?
Magonjwa ya akili ni matatizo ya
ubongo ambayo humfanya mtu
kuwa na hisia, fikira na matendo
tofautinayaleyanayotarajiwana
jamii na kushindwa kukabiliana
na changamoto za maisha.
husababishwa na Nini?
Magonjwa ya akili yanaweza
kusababishwa na sababu za
- kibaiologia au
- kisaikolojia;
Sababu za kibiologia
• Kurithi vinasaba kutoka kwa
wazazi.
• Magonjwa ya muda mrefu kama
degedege, malaria kali, UKIMWI
nk
• Matumizi ya dawa za kulevya
Sababu za kisaikolojia
• Majanga, ubakaji, uvamizi, ajali,
utekaji nyara, kukosa elimu,
kukosa ajira nk
• Kufiwa, kutengana,talaka, ugoni,
kufungwa
• Kufukuzwakazi,kukosamishahara,
kustaafu kazi nk.
• Kutokufanya vizuri kwenye
masomo na Kufukuzwa chuo/
shule
• Matatizo yanayowaathiri watoto
kisaikolojia
* Kunyanyaswa kingono
* Kupigwa na kutengwa
* Kutothaminiwa
* Kutokupata matunzo stahiki
Dalili za Magonjwa ya Akili ni Zipi?
Magonjwa ya akili yapo ya aina
nyingi na dalili zake zinatofautiana
kati ya ugonjwa moja na mwingine.
Dalili za Kihisia
• Kusikia sauti ambazo watu
wengine hawazisikii
• Kuona vitu ambavyo watu
wengine hawavioni
• Kuhisi kufuatiliwa na watu
• Wivu uliopitiliza
• Kuhisi mawazo yake
yanajulikana na watu wengine
au yanazungumzwa kwenye
vyombo vya habari
• Kuhisi kuwa mtu anatumia
mawazo yake kufanya mambo
Fulani
• Kuhisi harufu ambayo watu
wengine hawaisikii
• Kuhisi maisha hayana thamani
na kuona bora kufa kuliko kuishi
Dalili za Kimwili
• Kukosa furaha au kuwa na furaha
kupita kiasi
• Kuwa na wasiwasi au woga
kupita kiasi
• Kupunguzakuongeaau kuongea
kupita kiasi
• Hasira za haraka na kufikia hatua
ya kudhuru watu au kuharibu
vitu.
• Kuwa na msongo wa mawazo
• Kujitenga na watu na kupenda
kukaa mwenyewe muda mwingi
• Kutokuwa na ari ya kufanya kazi
au kufanya kazi nyingi kwa wakati
mmoja bila ya kuzikamilisha
• Kutokuonyesha hisia yoyote usoni
mwake [furaha au huzuni]
• Kutokujijali usafi na muonekano
wake
• Mwili kukosa nguvu au kuhisi mwili
una nguvu sana kupita kiasi
• Kukosa usingizi au kulala usingizi
sana kupita kiasi
• Kukosa hamu ya kula au kuwa na
hamu sana ya kula
• Kutokutulia (kuhamanika) au
kutulia sehemu moja muda mrefu
bila ya kujisogeza
• Maumivu sehemu mbalimbali
za mwili ambayo vipimo vya
hospitali havionyeshi tatizo lolote
la kimwili.
Dalili za Kiakili
• Kukosa umakini wa shughuli zake
za kila siku
• Kusahaukwaharakaaukupoteza
kumbukumbu
• Kukosa uwezo wa kupambanua
mambo kwa mitazamo tofauti
• Kutokujali
• Kuwa na imani zisizo za kawaida
kama vile;
* Kuwa mtu maarufu au Nabii
* Kupokea taarifa kutoka
kwenye redio au mitandao
ya simu
* Imani ya kuwasiliana na watu
maarufu
* Kuamini kuwa na nguvu ya
ziada kutoka nje ya mwili
*Imani kuwa kuna watu
wanamfuatilia/ wanataka
kumdhuru
• Mawazo yake hayana mtiririko
unaoeleweka.
Matibabu ya Magonjwa ya Akili
Matibabu ya magonjwa ya akili
hutoafautiana kati ya ugonjwa
mmoja na mwingine
- Elimu kwa jamii kuhusiana na
magonjwa ya akili ni kitu cha
muhibu sana katika kuzuia
kujirudia au kupata ugonjwa wa
akili, juu ya matibabu na msaada
anaohitaji mgonjwa ili kuendelea
na maisha yake ya kila siku.
2.Kupatiwa uchunguzi mapema
ili apatiwe tiba sahihi na ya
mapema
3. Tiba ya kisaikolojia (kujitambua
aliko, anapotaka kuwa na
kuamua kufanya mabadiliko
kwa kutegemea uwezo wake
mwenyewe
4. Tiba kimwili kutumia dawa za
hospitali
5. Matibabu kwenye nyumba za
upataji nafuu (Sober Houses)
6. Ushirikiano kati ya mgonjwa
familia na wataalamu wa tiba
huleta mafanikio makubwa sana
katika matibabu.
7. Kutokutumiamadawayakulevya
ikiwa ni pamoja na vilevi
8. Pata muda mrefu wa kupumzika
9. Fanya mazoezi
10. Usijitenge na jamii
11. Kujibidisha kwenye shughuli za
kuleta kipato
_1.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)